Makala Maalumu, by Happiness Team
HAPPINESS
MASSAGE SERVICES
Tunafurahi sana kukushirikisha bidhaa zetu bora, na jinsi bidhaa zetu
zitakavyoweza:-
·
Kukupa
afya bora
·
Kukufanya
ujihisi vema
·
Na
kukufanya uonekane kijana,kama ilivyo kwa maelfu ya Wasambazaji wetu na Wateja
wetu Duniani kote, ambao wamenufaika kutokana na kutumia bidhaa zetu.
Dhima yetu:
Ni kutoa bidhaa zenye ubora na sifa ili kuwawezesha watu waishi Maisha marefu
na yenye afya bora.
Katika Makala
hii ya uwasilishaji tunataraji kukupatia wewe Taarifa muhimu Juu ya kudumisha
afya njema ili uweze kufurahia na kunufaika na maisha yako.
Tuanze somo.
Moja ya sababu za Magonjwa hatarishi/ya
kudumu ambayo yanafahamika na binadamu leo hii hujulikana kama Free
radicals(radical huru).
Radical huru
huvamia mwili wa binadamu kwa kushambulia seli za mwili na hivyo kuzitia dhiki
katika utendaji wake wa kawaida. Hali hii huzifanya zibaki katika hali isiyo ya
kawaida na zenye afya duni.
Hivyo kama
seli zipo katika hali hiyo isiyo ya kawaida na zenye afya duni basi, Tishu za
mwili, viungo na hata Mfumo wa mwili kujumla huathirika pia.
Hivyo
kutokana na kuathirika kwa mwili baadhi ya magonjwa hatarishi hujitokeza,
Magonjwa hayo ni kama vile Magonjwa ya moyo, Kisukari na hata Kansa(Saratani).
Kwa bahati
mbaya sana kila siku tunashambuliwa na Radical huru kutokana vyakula visivyo na
virutubisho bora na kutokana na Ucahafuzi wa mazingira na Matumizi ya kemikali
ya kila siku ambayo yamekuwa kawaida kwetu na Msongo wa mawazo.
Cha
kusikitisha Zaidi, Miili yetu inaweza kuchukua radical huru hizo nyingi lakini
haina uwezo wa kuziondoa radical huru hizo zote na Mwishowe afya ya mwili
hudhorota.
Kwa bahati
nzuri, mwili w binadamu una Vikingamwili vingi dhidi ya hizi radical huru na
miongoni mwa vikingamwili hivyo kimoja Hufahamika kama Antioxdant(Kikingasumu).
Antioxidans(Vikingasumu)
huzifanya seli zilizoshambuliwa na radical huru zirudi tena katika hali ya
kawaida, imara na zenye nguvu Zaidi na seli huhifadhiwa hivyo zinaweza kufanya
kazi kufanisi na kwa usalama zaidi.
HATAHIVYO:Mwili
w binadamu hauwezi kutengeneza Vikinga sumu asilia muda wote. Mwili wa binadamu
unatakiwa upatiwe Vikingasumu hivi vya kutosha kwa ajili ya kupambana na athari
mbaya za radical huru.
Na vyanzo
bora kabisa vya Vikingasumu hivi ni Matunda na Mboga za majani.
Kwa hakika Shirika la afya Duniani (WHO) imependekeza kwamba watu wenye umri Zaidi nya miaka 35 wanatakiwa kula kwa
kiwango cha chini kabisa ni Matunda matano kila siku na mboga za majanai. Ili kuupatia
mwili virutubisho vya kutosha hususani Vikingamwili.
Hata hivyo
Mapendekezo haya yanaonekana kuwa ni changamoto kubwa kwa watu kutokana na
Mtindo mbaya wa Maisha usiozingatia kanuni za afya.

Leave a Comment